BI-SHOP MPEMBA:FAHAMU JINSI YA KUWA BILIONEA NA KUWA KIONGOZI BORA








Ili kuongeza ufahamu katika mambo mbalimbali hususani mambo ya ujasiliamali na uzalendo wa nchi lazima kila mtu asome vitabu vya kumjenga.

Rai hiyo imetolewa na mkurugenzi wa kituo cha redio cha kwa neema fm cha jijini Mwanza Dr:Bishop Augustine Mpemba ambaye pia ndiye askofu mkuu wa kanisa la Tanzania Field Evangelism(TFE)wakati akizunguza  katika  hafla  ya uzinduzi wa vitabu viwili  vya kulipenda taifa  na kulijenga na kitabu cha mawazo ya mabilionea.

Ili mtu yeyote  aweze kujikwamua kutoka  hatua moja kwenda hatua nyingine ni lazima aongeze maarifa  na kutambua wapi alikosea mwanzo na kufuta makosa ya mwanzo bila kukata  tamaa  na kujifunza jinsi wengine walivyo fanikiwa  kwa kusoma vitabu mbalimbali na kuongeza ufahamu”Alisema bishop Augustine Mpemba.
 Bi-Shop Mpemba
Katika hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa JB Belemonte Hotel jijini Mwanza na kuhudhuliwa na watu mbalimbali,bishop Mpemba aliongoza  uzinduzi  wa vitabu hivyo  ambavyo ameviandika mwenyewe na kutoa wito kwa jamii kuvisoma vitabu kwani vina manmbo mengi ambayo yatawajenga kiimani na kiuchumi pia. 

Akizungumuzia kitabu cha Kulipenda Taifa na Kulijenga Dr:Bishop Mpemba amesema kuwa kitabu hicho  kimekuja katika wakati muafaka ambapo taifa linahitaji viongozi imara,kupiatia kitabu  hicho jamii itafahamu jinsi ya kumchagua kiongozi bora wa nchi na kiongozi bora wa yeyote.
 
 “Nchi yetu ina viongozi wa siasa wengi na si viongozi bora,viongozi wa siasa huelekeza nguvu zao katika chaguzi zinazokuja,lakini kiongozi bora huelekeza nguvu  katika usitawi wa kizazi kijacho” alisema bishop mpemba  na kuiomba jamii kukisoma kitabu hicho ili imutambue kiongozi bora.

Kuhusu kitabu cha  Mawazo ya Mabilionea bishop Mpemba alisema kitabu hicho kinafundisha njia bora za namna ya kuwa bilionea na kuondokana na umasikini kwa kuzingatia mambo kazaa.

“tatizo kubwa linalo sumbua  jamii  ni kuwaza  njinsi ya kuanza hatua moja ya ulicho nacho na kukifanya kiwe kikubwa”alisema bishop Mpemba.

Aidha mhasisi yuho wa kituo cha kwa neema fm radio alihitimisha kwa kuiomba jamii imuunge mkono  iliaendelee kutoa vitabu vingi na kuendelee kuelimisha jamii hususani elimu ya ujasiliamali na uzalendo wa nchi.


-Kufahamu jinsi ya kuvipata vitabu hivyo,sikiliza maelekezo hapa chini
Share on Google Plus

About Promover

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment