Askofu Mkuu Wa Jimbo Kuu Katoliki Dar Es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo Amewaomba Watoto Wa Jimbo Lake Waende Mafia Wakahubiri Injili Ili Watu Wapate Kuokoka.
Akofu
Pengo Ameyasema Hayo Wakati Akiwaaga Watoto Jimbo Kuu La Dar Es Salaam Ifakara
Na Mpanda Katika Viwanja Vya Msimbazi Centre Jijini Dar Es Salaam Kabla Ya
Kuanza Safari Ya Kuelekea Mafia.
Safari Hiyo Imeanza Saa 1:42 Asubuhi
Ikiongozwa Na Askari Wa Usalama Barabarani Huku Takribani Watoto 800 Wakiwa
Wenye Furaha Wakiimba Na Kusali Na
Hatimaye Waliwasili Mafia Saa 11:30 Jioni.
Watoto Hao Wamepokelewa Na Askofu
Msaidizi Wa Jimbo Kuu Katoliki Dar Es Salaam Mhashamu Eusebius Nzigilwa Pamoja
Na Paroko Wa Parokia Ya Mafia Padri Francis Massawe.
Akiongea Padri Francis Massawe Amesema
Kuwa Mafia Ni Kisiwa Ambacho Asilimia 90 Ya Wakazi Wake Ni Waislamu Hivyo Kina
Changamoto Kubwa Katika Uinjilishaji Huku Akimuomba Kardinali Pengo Azidi
Kuhamasisha Vyama Vingine Vya Kitume Kwenda Kisiwani Humo Kuinjilisha.
Kutokana Na Sensa Ya Watu Na Makazi
Ya Mwaka 2013 Idadi Ya Wakristo Kisiwani Humo Ni 1693 Ila Hija Ya Utoto
Mtakatifu Kila Mwaka Imepelekea Waislamu 10 Kukubali Kumpokea Kristo Kwa
Kubatizwa.
0 maoni:
Post a Comment