RAIS wa Tanzania Dk. John Magufuli na
Mkewe Mama Janeth Magufuli wamemtembelea na kumpa pole Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu
Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.
Hatua hiyo ni kufuatia kifo cha Dada
yake aitwaye Efrazia Pengo aliyefariki dunia jana tarehe 22 Desemba, 2016
katika Kijiji cha Mwazye,Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa akiwa na umri wa
miaka 79.
Rais Magufuli na Mama Janeth Magufuli
wamemtembelea Kardinali Pengo katika makazi yake yaliyopo Kurasini Jijini Dar
es Salaam.
0 maoni:
Post a Comment