RAISI MAGUFULI NA MKEWE WAMTEMBELEA ASKOFU PENGO



  RAIS wa Tanzania Dk. John Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli wamemtembelea na kumpa pole Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.


Hatua hiyo ni kufuatia kifo cha Dada yake aitwaye Efrazia Pengo aliyefariki dunia jana tarehe 22 Desemba, 2016 katika Kijiji cha Mwazye,Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa akiwa na umri wa miaka 79.


Rais Magufuli na Mama Janeth Magufuli wamemtembelea Kardinali Pengo katika makazi yake yaliyopo Kurasini Jijini Dar es Salaam.
 
 
 
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment