Baadhi Ya Wachungaji
Na Waumini Wa Makanisa Yalioko Wilayani Geita Wamevamiwa Na Kupigwa Kwa Fimbo,Mikuki Wakiwa Ibaadani Kwa Madai Ya Kutotii Amri Ya Kuwataka Kucheza Ngoma Za
Jadi.
Amri Hiyo Ilidaiwa
Kutolewa Na Mwenyekiti Wa Kijiji Cha Lubanda,Kilichoko Kata Ya Busanda Elias
Mliyamali Kuwata Wasio Tii Agizo Hilo Kuhama Mara Moja Kijijini Hapo.
Akizungumza Mchungaji
Wa Kanisa La Evangelical Assemblies Of God Tanzania(Eagt) Elia Antony Amesema
Amesikitishwa Na Amri Ya Mwenyekiti Huyo Kuwalazimisha Kufanya Mambo Ambayo
Yapo Kinyume Cha Imani Yao.
Mchungaji Antony
Amesema Ngoma Za Jadi Zilikuwapo Tangu Awali Na Viongozi Waliopita Wala
Hawakufanya Hivyo Kulazimisha Watu Kwa Kuwa Kila Mtu Ana Imani Yake.
Kwa Upande Wake
Askofu Cpct Mkoa Wa Geita Stephano Saguda Amesema Alipozipata Taarifa Hizo
Alizifikisha Kwa Mkuu Wa Wilaya Ambaye
Aliahidi Kulifuatilia Jambo Hilo Na Kutoa Waraka Maalum Kwa Mwenyekiti Huyo Wa
Kijiji.
Chanzo:Jibu la Maisha
0 maoni:
Post a Comment