MAMA MCHUNGAJI AJIFUNGUA MAPACHA GEREZANI AKISUBIRI KUNYONGWA HUKO NCHINI CHINA


Habari za kusikitisha kutoka China zinaeleza kuwa mtanzania mmoja Bi:Celina John aliyekamatwa kwa tuhuma za kuingiza dawa za kulevya nchini China mwishoni mwa mwaka jana akiwa sambamba na aliyekuwa mmewe mchungaji John Mangale ambaye alinyongwa katika tukio hilo,amejifungua watoto mapacha na sasa amepewa muda kidogo anyonyeshe kisha naye anyongwe na haijafahamika ikiwa watoto waliozaliwa gerezani watakuwa raia wa China na kulelewa na taifa hilo lenye imani kali za kuzuia uzazi atarejeshwa nchini.

Habari za uhakika kutoka kwa mtu wa karibu na Celina zinasema kuwa,mama huyo aliyekamatwa na mmewe wakiwa pamoja na mtoto wa miaka minne aliahirishiwa adhabu ya kunyongwa kwa kuwa alibainika kuwa alikuwa mjamzito na akaamuliwa na serikali ya Uchina kuwa atasalia gerezani hadi atakapojifungua na kupewa muda wa kunyonyesha kisha atanyongwa.

Nyakati linafahamu kuwa John aliwahi kuhudumu katika kanisa la Breakthrough Assemblies of God lenye makao yake makuu Boko jijini  Dar es salaam,kwa muda lakini miezi saba hivi kabla ya kutoweka aliaga kuwa anakwenda kufungua huduma yake sehemu nyingine,hakuonekana kwa muda hadi pale taarifa zilipoibuka kuwa amekamatwa na madawa hayo “unga” nchini China na kunyongwa.

Uchunguzi wa Nyakati umebaini kuwa licha ya mchungaji aliyenyongwa kuwa na mtoto wa miaka mine aliyesafiri naye pia ana binti mwingine(jina limehifadhiwa)ambaye yuko darasa la saba na mtoto aliyekuwa na wazazi wake China tayari alirejeshwa jijini Dar es salaam kwa msaada wa ubalozi wa Tanzania nchini China na kukabidhiwa kwa jamaa zake.

Juhudi za kumpata mchungaji Gozbert Simtomvu kuzungumzia habari za mama huyo aliyekuwa muumini wake kujifungua na kusubiri kunyongwa  hazikufanikiwa lakini wakati mchungaji John aliponyongwa alinukuliwa na gazeti moja la kila wiki(sio Nyakati)akikataa kuthibitisha kuhusu madai hayo,lakini alikiri kusikia taarifa hizo ambazo ziliwaliza waumini wengi kwa vile mchungaji alikuwa mwanafamilia. 
Licha ya mama huyo,taarifa zimesema kwa wapo watanzanzania wengine wengi waliokamatwa na dawa za kulevya ambao wanasubri kunyongwa katika magereza mbalimbali ya China has a yale ya HongKong na hivi karibuni waliandika waraka mrefu wa kutaka watanzania wengine wasijaribu kufanya biashara hiyo.


Chanzo: Gazeti la Nyakati
Share on Google Plus

About Jacktan Msafiri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment