Kwaneema fm radio inakuarika
kushiriki katika kampeini ya 'jenga mnara' kampeini yenye lengo la kukusanya Tsh
mill 100 hadi kufikia mwezi dec kwaajili ya kujenga mnara wa kurusha matangazo
ya radio ili kuweza kuwafikia watanzania wengi iwezekanavyo.
Kutokana na mahitaji makubwa ya
uendeshaji pesa imeendelea kuwa changamoto kwetu hasa katika kulipa mnara
ambapo kila mwezi kiasi cha dola za kimarekani 1000 huhitajika na kusababisha
kuchelewesha mipango mingine ya kuendelea kuifikia jamii ambayo haipo katika
masafa yetu kwa sasa.
Malengo ya muda mrefu tuliyonayo Kwa
Neema Fm redio ni pamoja na Kuongeza masafa ili kuifikia jamii yenye kiu ya
mabadiliko ya roho,nafsi na mwili ambapo katika miaka mitatu tunaamini kupanua
wigo wetu katika nchi yetu ili kuzipeleka Habari Njema katika sikio la kila
mtanzania.
Kwa neema redio imelenga Kujenga mnara
wake ili kupunguza gharama za kukodi mnara na imelenga kuifikia jamii kwa
njia ya miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo itasaidia kuimarisha maisha ya
kila mtanzania.
Tuma mchango wako wa mara kwa mara kwa
njia ya M-pesa kwenye namba 0753982982 na mungu akubariki.
SASA
IFAHAMU KWANEEMA FM RADIO.
Kwa Neema Fm ni kituo cha redio cha
Kikristo chenye maono ya Kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu kwa
watu wote na ni Kituo kinachopatikana katika masafa ya 98.2 MHz yakiwa ni
matokeo makubwa ya maono ya Kanisa la Tanzania Field Evangelism chini ya Mtumishi
wa Mungu Balozi wa Ufalme Bishop Dokta Augustine Mpemba.
Baada ya juhudi kubwa na kujitoa kwa
mali na maombi kanisa lilipewa kibali cha kufungua redio ya Kwa Neema Fm chini
ya kifungu cha 13 cha sheria ya Vyombo vya Habari mnamo tarehe 11/3/2010.
Mnamo Julai 03 2010 jiwe la msingi
liliwekwa naye Askofu Mkuu wa kanisa la Crossroad la huko Marekani ambapo hafla
hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini, siasa na wa taasisi zisizo za
kiserikali.
Kuanzishwa kwa redio ya kwa neema
kumebebeba misheni kubwa ya kuhubiri uhitaji mkubwa wa mwanadamu kuacha
maisha ya dhambi ili akombolewe na kufunguliwa kutoka katika minyororo ya
Shetani kwa kutumia Maandiko Matakatifu ya Biblia.
Kwa Neema Fm inatumia jukwaa hilo la
hewani katika Kushuhudia na kulitangaza Jina la Yesu Kristo,Kumhubiria
mwanadamu kuacha maisha ya dhambi na Kutangaza kwa jamii kubadili tabia
zisizofaa zinazopelekea maambukizi ya VVU/UKIMWI na Kuhabarisha na
kuelimisha kwa kutumia habari za kijamii na kimaadili kwa maendeleo umma.
Kwa Neema Fm redio inaheshimu watu wote
wa dini na madhehebu mbalimbali na inaamini katika neema ya Yesu kristo
iliyoaachiliwa kwa watu wote.
Pamoja na hayo yote Kwa Neema fm redio
inatoa mafundisho yenye nia ya kubadilisha maisha ya watu katika mtazamo wa
Kiroho, kinafsi na kimwili ili kuijenga jamii yenye afya kijamii, kimaadili,
kisiasa na pia kiuchumi.
Baada tu ya kuanza kurusha matangazo
yake Kwa Neema Fm redio imejijengea kiasi cha wasikilizaji milioni moja na nusu
ikiwa inafika wilaya mbili za Mwanza mjini ambayo ni Ilemela na Nyamagana, pia
Nansio Ukerewe, wilaya ya Sengerema, Magu, Misungwi na Kwimba lakini pia
inasikika katika Mkoa wa Geita, Shinyanga Kahama, Mara Bunda, Musoma vijijini
na wilaya ya Mugumu.
Kikiwa na miaka mitano(6) ya utendaji
kazi kwa mkoa wa Mwanza na maeneo jirani tumeshuhudia watu wakiokoka,
kuponywa, kufunguliwa na kukua kiufahamu katika mambo ya Kiroho na maisha ya
jamii yakibadilishwa katika wema.
Kwa namna ya ajabu shuhuda
nyingi zimekuwa zikitolewa na watu wa madhehebu mbali mbali kuhusu redio hii
ilivyobadilisha maisha yao kupitia vipindi vya mafundisho ya kiroho na
kijamii huku shukrani zikitolewa kutoka kwa viongozi wa ngazi zote kwa jinsi
ambavyo vipindi vya redio hii vinavyoelimisha jamii katika kupambana na ujinga,
umaskini na maradhi.
Kwa Neema Fm imeendelea kufanya
kazi kwa ubunifu na ufanisi katika vipindi vyake ili kufanikisha maono haya
makubwa kwa ajili ya Ufalme wa Mungu.
Hadi sasa Kwa Neema fm redio ina jumla
ya watendakazi 14 wakiwemo watangazaji 10 ambao wanafanya vipindi zaidi ya 15.Kati
ya vipindi tulivyonavyo ni pamoja na Amka uangaze ambacho huanza asubuhi njema
kwa Neno la Mungu na mafundisho mbalimbali ya kiafya, kimazingira, kiusalama,
kijamii na kisiasa.
Fikra Pevu:kipindi chenye mafundisho ya kibiblia, kisaikolojia na
uraia ambacho huruka asubuhi baada ya amka uangaze
Yaliyosheheni: ni kipindi chenye kuijuza jamii yale yanayoendelea katika
jamii kimatukio,Full Shangwe ni kipindi burudani za kiufalme ambapo habari
zinazohusu muziki wa injili hupatikana hapo na Kutoka Chumba cha habari
ambacho hulenga magazeti na mada mbalimbali pamoja na matukio na Taarifa za
habari ambazo zimegawanywa kuhakikisha kila wakati watu wanahabarishwa
Vipindi vingine ni Kona ya Michezo ,Majira
ya Ufahamu Na Bishop Augustine Mpemba ambacho huwatoa watu matongotongo
ya ufahamu wa neno la Mungu, Msasa wa wiki Kipindi kinachojadili
mada za kisisasa, kijamii na kiuchumi.
Fumbua Macho kipindi cha maarifa ya kibishara na ujasiriamali
Vipindi vya Afya Mazingira, wanawake
watoto vijana na vingine vingi.
Timu hii ya watendakazi imeendelea
kufanya kazi kwa ubunifu mkubwa ili kuboresha kazi hii na kutimiza malengo ya
maono haya ya kiufalme.
Katika muda huu wa miaka 6 Kwa Neema Fm
redio imeweza kufanikiwa kufanya yafuatayo Kwa Neema Fm kupitia kipindi
cha Kwa Neema (kama kilivyojulikana wakati huo sasa kinaitwa Majira Ya Ufahamu)chini
ya Mwalim wa Neno la Mungu Bishop Augustine Mpemba akishirikiana
na walimu wengine wa Theolojia walijikita katika kufundisha kweli ya Maandiko
matakatifu na kufichua fundisho hilo potofu ambalo liliwataka watu kuwa na
maji, vitambaa au mafuta ili kupata matokeo ya maombi yao.
Katika fundisho hilo kipindi hiki
kilifichua pia watumishi watumiao nguvu za giza ili kuwaombea watu na wale
wanaotaka fedha ili kuwaombea watu.
Kutokana na watu wengi kusikia mafundisho
haya shuhuda zilimiminika kuelezea ukweli wa mafundisho hayo potofu,na shukrani
zilimwagwa kwa redio ya Kwa Neema Fm kwa kuleta mwanga katika maisha ya watu.
Watu wengi walishuhudia jinsi walivyoathiriwa kifedha na kisaikolojia na
watumishi waliotumia mahitaji yao kujinufaisha.
Pamoja na hayo Kwa Neema Fm ilifanikiwa
kushiriki katika kutoa mwamko wa watu kushiriki katika Sensa ya watu
iliyofanyika 2012 na pia katika kutoa taarifa za matokeo ya sensa hiyo. Katika
hatua zote redio hii imeshiriki kuwahamasisha watu kushiriki utoaji wa
maoni katika Upatikanaji wa rasimu ya Katiba mpya ya Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
Katika uchaguzi wa Mwaka 2010 Kwa Neema
Fm redio ilishiriki kuhamasisha watu kujitokeza na kupiga kura ili kuweza
kuwapata madiwani, wabunge na hata Rais wanayemtaka Katika mwaka wa 2011
kupitia hekima na maarifa ya Mwasisi Bishop Mpemba Kwa Neema ilifanikiwa
kuanzisha Partners club ambayo ilikusanya watu kutoka madhehebu mbalimbali
wenye mapenzi mema na ufalme ambao walikubali kusupport maono haya kwa
kuchangia fedha kila mwezi. Katika hili tulipata kujua kuwa Ufalme ni Mkubwa
kuliko ukubwa wa madhehebu yetu kwani watu wenye kutoka majengo mbalimbali ya
ibada walinia kuusimamisha ufalme wa Mungu na kusupport kazi hii pasipo
mitazamo ya udini.
Baada ya kufungiwa miezi sita ikiwa ni
adhabu iliyotolewa na Mamlaka ya mawasiliano Tanzania kutokana na ukiukwaji wa
sheria za utangazaji, Kwa Neema ilijipanga upya na kuwahakikishia viongozi wa
TCRA makosa kama hayo hayatajirudia tena na mnamo mwezi wa nane mwaka 2013
redio Kwa Neema Fm iliendelea kurusha matangazo yake tena na katika muda mfupi
Tuliandaa Tamasha kubwa la shukrani ambalo lilinia kumshukuru Mungu kwa Miaka 3
ya kuwa hewani pamoja na kuwashukuru wadau wetu wote.
Tamasha lilionesha kwa kiasi kikubwa
mapenzi ya watu na redio hii ya Ufalme ambapo katika tamasha hilo
tuliweza kupata wadhamini 11 ambao walijitoa katika kufanikisha shughuli nzima
na pia kuhudhuliwa na watu zaidi ya elfu 6000 katika uwanja wa CCM Kirumba.
Tamasha ni moja ya mafanikio ya kazi
hii nzuri ambayo inagusa maisha ya watu na Kupitia hilo tuliweza kupata wadau
wapya lakini pia partners wapya kwa ajili ya kusupport kazi hii ya Ufalme.
Baada ya kuandaa Tamasha hili la
shukrani na kuona ukarimu na upendo wa watu wa kanda ya ziwa Kwa Neema Fm
iliamua kuandaa Tamasha jingine lililobeba nia ya kuyafikia makundi yenye
uhitaji ambayo yamezunguka jamii yetu na kuwagusa katika mahitaji yao muhimu
kama vile chakula na mavazi.
Kwa kushirikiana na mfuko wa Pensheni
wa LAPF, Tulifanikiwa kukusanya makundi matano ambayo ni Makundi ya waathirika
wa VVU/UKIMWI, wajane, yatima, walemavu na familia zinazoishi kwenye mazingira
magumu.
Na katika hili watu walijitoa kwa
michango ya mavazi na pesa ambazo zilikusanywa na kuwezesha manunuzi ya vyakula
kama vile Mifuko 45 ya Mchele, Mifuko 45 ya unga mifuko 10 ya sukari ndoo 10 za
mafuta, dumu za litre 5, 10 za mafuta, Ndoo 10 za sabuni ya unga pamoja na
mahitaji mengine ya muhimu.
Hili ni Tamasha ambalo liliileta
Kwa Neema fm redio katika maisha ya jamii.Watu wengi wameendelea kuipongeza
redio kwa kuifikia jamii ambayo inatamani kutambuliwa na kuhudumiwa.Tamasha
hili pia lilidhaminiwa na wadhamini 14
Pamoja na hayo yote Kwa Neema Fm
imeendelea kung’ara katika vipindi vyake mbalimbali kama vile taarifa za
habari, vipindi vya burudani ya kiufalme,vipindi vya kuelimisha jamii na
vipindi vya michezo.
Ni ukweli usiopingika kwamba Mungu
ndiye atendaye kazi pamoja nasi katika kutupatia mema ambayo yataleta matumaini
katika jamii inayotuzunguka.
Aidha kwa neema redio inatambua
mchango wa kila mmoja na akiwepo Bishop Mpemba na Mkewe Dinnah Mpemba
Kanisa la TFE, maaskofu na wachungaji wote wa Mwanza, viongozi kutoka Mamlaka
ya Mawasiliano Tanzania viongozi wa Serikali, Partners wote wa redio wadau wote
wa Kwa Neema Fm na kwa moyo wa dhati kwa makampuni na taasisi ambazo hazikusita
tulipowaendea kwa udhamini wa matamasha yetu ambao ni LAPF mfuko wa Pensheni,JB
Belmont Hotel,Grace Product Limited,TING HD( Agape Ministry),Semira
Electronics,Impression Limited,Lake Oil filling station,Mama Nyimbo
decoration,Kassa Charity Schools,Moil Filling station,Narae Day Care centre ,Dr
Jumanne Mhazini ( Huduma ya uponyaji),Nyanza Bottling Company,Star of Jerusalem
clinic,Encouragers Image,Lawra Cakes,Joshua Dede mapazia ,Great Zone
Entertainiment ,VIP Beauty Saloon,Isamilo Express na AM
limited,Promover.com
Sherehe hiyo ilihudhuriwa na wageni
waalikwa kutoka sehemu mbalimbali na watu walifurahia vitabu hivyo
vilivyoandikwa kwa utaalamu na kiwango cha juu na ni vitabu vilivyo zinduliwa
rasmi na Bi:Victoria John na Ana Tiba waliokuwa wageni rasmi wa siku hiyo.
Imetolewa na:
KWA NEEMA FM RADIO
98.2
MHz
P.O. Box 1301 Mwanza, Tanzania
Tel: +255 282 561 390
0r 0712-276920
E-Mail:
kwaneemafmradio@gmail.com
0 maoni:
Post a Comment