Kikundi cha muziki wa injili kutoka jijini Mwanza nchini
Tanzania kinachojulikana kama Kihayile Group kimechaguliwa kushishiriki katika
tuzo kubwa kabisa za nchini England(London uingeleza) zinazojulikana kama AGMMA
2017 yaani African Gospel Music & Media Awards.
AGMMA ni tuzo kubwa kabisa ambazo hutolewa nchini uingeleza
kwaajili ya kutambua mchango mkubwa wa waimbaji wa nyimbo za injili pamoja na wadau
wengine wanaotoa mchango mkubwa katika masuala ya injili maeneo mbalimbali
ulimwenguni.
Akizungumza katika uzinduzi wa tuzo hizo mapema mwezi wa
January Bwn:Charles Korateng mwanzilishi
wa tuzo hizo ambaye pia ni mkurugezi wa
1615 Media ambayo ndio kampuni inayoandaa tuzo hizo,alisema tuzo za mwaka huu
azitahusisha tu waimbaji wa muziki wa injili bali zitaenda mbali Zaidi kwa
kutambua mchango wa wanablog,Radio na Tv za mtandaoni pamoja na watumishi wa
Mungu wa makanisa madogo madoo wanaosukuma injili kwa njia mbalimbali.
Zoezi la kuwapigia kura washiriki wa tuzo hizo limefunguliwa
rasmi tar 31/3/2017 na litafungwa rasmi usiku wa tar 21/5/2017 Ambapo
ukiachilia mbali Kihayile Group watanzania wengine waliochaguliwa kushiriki
tuzo hizo ni Angel Benard pamoja na Christina Shusho na kutoka nchini Kenya ni
Mercy Masika.
Wakizungumza na Promover.com Kihayile Group wamesema
wanayofuraha kubwa sana kuchaguliwa kushiriki katika tuzo hizo ambapo
wamewaomba wanamwanza na watanzania kwa ujumla kuwapigia kura ili waweze kuleta
tuzo nyumbani.
Ili kupiga kura katika tuzo hizo utatakiwa kujaza email yako
kasha kuchagua unayempigia kura,ambapo unaruhusiwa kupiga kura mara moja tu kwa
email moja.Kuwapigia kura moja kwa moja Kihayile group tafadhali fuata link kisha chagua namba 15>> HAPA
Hafla ya utoaji wa Tuzo hiyo itafanyika 3/6/2017 Kwenye
ukumbi wa Stratford Circus
Centre,jijini London Uingeleza.Kwa maelezo Zaidi fungua>> HAPA
0 maoni:
Post a Comment