AICT KISEKE CHOIR WAFANYA TAMASHA KUBWA LA UZINDUZI WA ALBUM YAO YA VIDEO

Jumapili ya tar 4/11/2016 ilikuwa siku nzuri kwa kwaya ya AICT KISEKE ya jijini Mwanza,baada ya kwaya hiyo kuzindua rasmi album yao ya video inayojulikana kama WATU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA.

Uzinduzi huo umefanyika katika Tamasha kubwa kabisa lililofanyika katika kanisa la AICT KISEKE lililopo wilayani Ilemela jijini Mwanza.

Album hiyo imebeba jumla ya nyimbo 10 ambazo zote zimefanyiwa video na sasa imeingia sokoni na itaanza kupatikana mtaani.

AICT KISEKE CHOIR ni moja kati ya kwaya kongwe kabisa nchini Tanzania ikiwa imeanzishwa mwaka 1992 jijini Mwanza.Karibu sasa utazame picha za uzinduzi wa album hiyo.

-Sikiliza/Download hapa chini wimbo uliobeba album hiyo uitwao WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA:

Moja kati ya video kwenye album hiyo iliyozinduliwa itakujia baadaye kupitia kwenye tovuti hii.Taadhali endelea kututembelea.
Share on Google Plus

About Jacktan Msafiri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment