Je!uliipata
ile taarifa ya mchungaji huko afrika kusini kupulizia waumini dawa ya kuua mbu
machoni akidai ni tiba? kama uliipata hiyo basi kuna ripoti mpya kutoka huko
huko afrika ya kusini ambapo wakati huu sasa mchungaji anawanywesha waumini
dawa ya kuua bakteria aina ya Dettol ambayo nchini Tanzania hutumika zaidi
kusafishia chooni.
Mchungaji
maarufu kwa jina la Rufus Phala kutoka kanisa la AK SpiritualChristian lililopo
Makgodu,Limpopo,AfrikaKusini amewashangaza watu kwa kitendo cha
kuwanywesha Dettol waumini wake ilihali ina madhara kwa
binadamu.
Kwa
mujibu wa Daily Sun SA, mchungaji huyo alifanya kitendo hicho kwenye ibada za
kawaida kanisani kwake akiwataka waumini wenye matatizo na wanaohitaji maombi
wanywe Dettol aliyokuwa ameishika mkononi mwake huku akiwambia watapona shida
zao ikiwemo magonjwa.
“Nafahamu
kuwa Dettol ni sumu, lakini Mungu ameniagiza niwape na muitumie. Mimi nilikuwa
wa kwanza kuinywa,” – Mchungaji.
Pia
alisema kuwa amepokea meseji za WhatsApp kutoka kwa watu waliokunywa na
wamethibitisha kupona. Baada ya kuwepo kwa taarifa hizo, amehojiwa Daktari
kutoka Afrika Kusini, Dr Mabowa Makhomisane, ambaye amekiri kuwa Dettol ina
madhara inapotumika tofauti na maelekezo ikiwemo kuinywa
“Mtu
akinywa Dettol na ikafika tumboni, kimsingi hupunguza mzunguko wa hewa ya
Oxygen mwilini. Hali hiyo ikitokea mtu anaweza kupoteza fahamu na kufariki.
“Na kama mtu atatapika na bahati mbaya maji maji yakaingia kwenye mapafu yake, Detto itamsababishia ugonjwa wa Nimonia. Mapafu yatajikunja na mtu atashindwa kupumua”
“Na kama mtu atatapika na bahati mbaya maji maji yakaingia kwenye mapafu yake, Detto itamsababishia ugonjwa wa Nimonia. Mapafu yatajikunja na mtu atashindwa kupumua”
Dr
Makhomisane amewashauri watu waliokunywa dawa hizo waende Hospitali kupata
vipimo ili kujua madhara waliyopata.
Kama
ulipitwa na ile ya dawa ya mbu ipitie sasa hapo chini:
0 maoni:
Post a Comment