Hayawi Hayawi sasa yamekuwa,lile tukio kubwa kabisa
lililokuwa likisubiriwa kwa hamu na wengi hatimaye siku imewadia.
Si kingine bali ni harusi ya mwimbaji mahiri wa nyimbo za
injili kutoka nchini Tanzania anayefahamika kwa jila la Madam Flora ambaye
atafanya sherehe kubwa ya harusi tar 30/4/2017 katika ukumbi wa Kishimba Beach
iliyopo mkabala na Rock Beach Garden jijini Mwanza nchini Tanzania kuanzia
majira ya saa 11:00 jioni.
Madam Flora anawakaribisha watu wote kwenye sherehe hiyo ya
aina yake ambapo siku hiyo itaambatana na uzinduzi wa album yake mpya kabisa
inayokwenda kwa jina la 'WAKATI WAKE' lakini pia kitabu kipya kinachoitwa 'SIRI ZA
FLORA MBASHA' kitazinduliwa katika sherehe hiyo.
Kadi za harusi hiyo zinapatikana kwa Tsh.50,000/=Single na
Tsh.70,000/=-Double.Kadi zinapatikana kwenye hotel ya Belmont Fair Mount Hotel
zamani JB Belmont Hotel,wahi sasa kadi yako maana kadi ni chache na hazitauzwa
mlangoni siku ya sherehe.
Waimbaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania
watakuwepo ambapo Madam Flora ataimba nyimbo zake zote kali Live katika sherehe
hiyo.
Vazi la sherehe hiyo ni rangi nyeupe hivyo basi unaombwa
kuja ukiwa umevalia rangi nyeupe.Kwa Mawasiliano Zaidi piga simu namba
0758105014/0655105014.Watu wote mnakaribishwa!
0 maoni:
Post a Comment