PADRI AJIUZULU BAADA YA KUKIRI KUMTONGOZA MTAWA


Padri wa ngazi ya juu katika makao makuu ya kanisa Katoliki ya Vatican anayetuhumiwa kukiri kumtongoza mtawa amejiuzulu. 

Taarifa hiyo imetangazwa jana na Vatican. Padri huyo raia wa Austria Hermann Geissler amejiuzulu kama mmoja wa viongozi wa juu katika taasisi inayoshughulikia mafundisho ya imani ambayo inafuatilia maadili ya kikatoliki. 

Taarifa ya Vatican imesema Padri huyo ameamua kuchukua uamuzi wa kujiuzulu ili kuzuia uharibifu ambao umeshafanywa kwa waumini na jamii yake.

Mchakato wa sheria za kidini zinazohusu adhabu uliofanyika 2014 ulimpa onyo padri Geisler baada ya mtawa wa zamani Doris Wagner kumtuhumu kuwa na tabia zisizofaa wakati wa kuungama.

Mtawa huyo alisema aliwekwa kwa masaa mengi akiwa amepiga magoti huku padri huyo akimueleza kwamba anampenda kimapenzi na hata kama hawaruhusiwi kuoana wanaweza kutumia njia nyingine.

Source:DW


Share on Google Plus

About Promover

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment