PAPA FRANCIS ATOA UJUMBE MZITO KATIKA ZIARA YAKE YA KWANZA YA KIHSTORIA UARABUNI


Kiongozi wa kanisa Katoliki Papa Francis anahitimisha ziara yake ya kihistoria katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na anatarajia kuongoza misa waumini wa kanisa Katoliki nchini humo.
Papa Francis amepongeza Umoja wa Falme za Kiarabu kwa kutokuwa na ubaguzi wa kidini na kusema kuwa nchi hiyo inatakiwa kuwa mfano kwa mataifa mengine yenye ubaguzi wa kidini.
Pia amekaribisha juhudi za Umoja wa Falme za Kiarabu kwa kuwapa ajira wahamiaji ambao wengi wao ni kutoka Ufilipino na India.
Umoja wa Falme za Kiarabu una wakazi zaidi ya 85% ya wahamiaji. Raia kutoka nchi za Asia ni asilimia 65 ya wakaazi wa nchi hiyo na wameajiriwa katika sekta zote, kuanzia ujenzi hadi katika hoteli.
Takribani Wakatoliki milioni moja wanaishi katika Umoja wa Falme za Kiarabu, sawa na mkaazi mmoja kati ya kumi.
Umoja wa Falme za Kiarabu una makanisa nane ya Katoliki,ambayo ni idadi kubwa ya makanisa Katoliki katika kanda hiyo.
Ziara hiyo ya kiongozi wa kanisa Katoliki duniani ni ya kwanza kuwahi kufanywa na kiongozi wa kanisa hilo kwenye rasi ya Uarabuni.


Lengo ni kufungua ukurasa mpya katika uhusiano baina ya wakristo na Waislamu.

Mrithi wa mfalme wa Abu Dhabi Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan alimpokea Papa Francis kwenye uwanja wa ndege akiwa na tabasamu huku akiongozana na mawaziri wake. 

Imam mkuu wa msikiti maarufu wa Al-Azhar wa nchini Misri, Ahmed el Tayeba pia alikuwapo uwanja wa ndege kumlaki Baba Mtakatifu.

Papa Francis na imam el Tayeb watahutubia kwenye mkutano utakaohudhuriwa na wawakilishi wa dini zote. 

Waumini wapatao 135,000 wanatarajiwa kuhudhuria misa hiyo ya hadharani.
Share on Google Plus

About Jacktan Msafiri

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment